Thursday, May 30, 2013

RIPOTI YA DAKTARI JUU YA KILICHOSABABISHA KIFO CHA MSANII WA BONGO FLAVA ABERT MANGWEA!


  Kwa mujibu wa ripoti hiyo kutoka hospitali alikopelekwa marehemu Ngwair, Dkt. Shirley Radcliffe amethibitisha kuwa kilichomuua Albert Mangwair ni sumu ya kilevi. [Ufafanuzi wangu] Kilevi au alkoholi inayolewesha watu kwenye pombe ni sumu. Ukiinywa kwa kiwango kikubwa, kinaweza kukusababishia upotevu wa fahamu, kupunguza uwezo wa kupumua, na hata kifo.
Taarifa hiyo inaendelea kwa kusema kwamba baada ya kunywa kupita kiasi, Ngwair alitumia mihadarati kwa kiwango kikubwa kuliko mwili wake unavyoweza kuhimili(drug overdose)iliyoko kwenye pombe. Dkt Radcliffe aliongeza kuwa Ngwair alipelekwa katika wodi ya watu mahututi kutokana na upungufu mkubwa wa oksijeni mwilini au “hypoxemia.”
Mmoja wa rafiki zake alikuta chupa mbili za vodka zikiwa tupu ndani ya gari, na Ngwair alikua na tatizo la kula linaloitwa bulimia kwa miezi kadhaa kabla ya kifo chake, ambapo alikua akijirusha bila kikomo bila kupumzika au kupumzika kidogo.
Sampuli ya kutoka tumboni kwake inaonyesha mchanganyiko wa kiwango kikubwa cha mihadarati aina ya cocaine, na heroine, na pia alikutwa akiwa na gramu 0.08 za bhangi kwenye damu.
Kifo chake kilisababishwa na massive heart attack (shambulizi la moyo?) na kushindwa kupumua, vilivyosababisha moyo wake usimame na akafariki baada ya sekunde kadhaa

No comments:

Post a Comment