Monday, June 24, 2013

SIWEZI KUSAHAU KISA HIKI

Ilikuwa mwezi wa 10 mwaka 2005 nilipojiunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam kusoma shahada yangu ya kwanza ya Sayansi katika Uhandisi wa Kompyuta na Teknolojia ya Habari (Bsc. in Computer Engineering and IT). Mimi pamoja na vijana wenzangu tuliotoka kwenye familia zilizo na uwezo wa kawaida sana na ambao ki msingi ni familia za wakulima za huko vijijini hapa nchini tulikuwa na wakati mgumu kidogo kuendana na mazingira ya chuo kikuu na jiji la Dar es Salaam kwa ujumla. Wanafunzi wa kiume waliochaguliwa kusoma shahada hii wengi wetu tulipewa vyumba vya malazi (accommodation) katika ghorofa moja pale kampasi kuu (main campus) jengo namba 2 (hall 2) ghorofa ya 7 na 8 (7th and 8th floor). Baada ya kujiunga na chuo tulitegemea kuanza kupatiwa sehemu ya mkopo kwa wanafunzi kwaajili ya chakula, malazi na vifaa vya kusomea (meal, accommodation and stationary) wakati huo ikiwa ni asilimia mia (100%). Badala yake mkopo huo ulichelewa kwa zaidi ya wiki mbili na kusababisha adha kubwa kwa wanafunzi pale chuoni. Ilitulazimu kuanza kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki ili kupata walau vijisenti vya kujikimu. Bahati mbaya mkopo uliendelea kuchelewa hadi kufukia kiasi wanafunzi kuanzisha mgomo mkubwa ukiongozwa na Raisi wa serikali ya wanafunzi (DARUSO) na waziri mkuu wake, wakati huo Mwita Waitara na John Mrema. Sikuchache kabla ya mgomo huo sisi tulianzisha mtindo maarufu wa KUPUNGUZA KULA KUBANA MATUMIZI uliokuwa ukiitwa "KUPIGA DESH ama PASI NDEFU", siku moja nilijikuta nikipiga pasi ndefu sana hadi nikadhoofika, nikaacha vipindi darasani na kwenda chumbani HALL II kulala, kwa bahati mbaya ama nzuri mwenye funguo wa chumba hakuacha funguo mahali ambapo huwa tunaweka, ikanilazimu kwenda kulala chumba cha jirani kwa rafiki yangu Musa Chibali Semwenda niliyekuwa nikisoma naye darasa moja pamoja na Edgar Tenga, Beatus FK, Linda Joseph, Irene Dubi Makundi, Paul G Mandu, William Nzunda, Hellen Maziku, Irene Kemilembe Joseph, .... Kilichotokea baada ya kulala sikupata fahamu tena. Baadae nimekuja kuzinduka Musa Chibali Semwenda ananinywesha chai na mkate. KUMBE NILIZIMIA KWA NJAA!. Baada ya kupata chakula kile nilipata nguvu kidogo na kisha kwenda zahanati ya chuo na daktari akaniambia ulikuwa umekaa muda mrefu sana bila kula. Mgomo ulipoanza nilishiriki kikamilifu huku nikiwa na maumivu makubwa moyoni kwamba ningekufa kwa njaa mie kama sio kusaidiwa na rafiki mwema. POLICE WANGENIPIGA NA KUNIUA KWA RISASI AMA MABOMU LAKINI NILIKUWA NAJUA NINACHOTETEA.
"SINTOACHA KUPAMBANA KUTETEA WANYONGE WENZANGU HADI PUMZI YANGU YA MWISHO"
Hizi ni salamu kwa Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mtoto wa Mkulima aliyesahau Wakulima wenzie kwa ulevi wa Madaraka) kauli yako ya juzi imezidi kunitia maumivu, na kunikumbusha yale mabomu tuliyopigwa na police miaka 8 iliyopita.

No comments:

Post a Comment