Mlipuko unaodhaniwa kutokana na bomu la kurushwa kwa mkono umetokea
katikati ya ibada katika kanisa katoliki la Mt Joseph lililopo Olasiti
Jijini Arusha ambako kwa siku ya elo kulikuwa na ibada ya Kuzindua
Parokia ya Mt Joseph Olasiti. Mlipuko huo unaelezwa kutokea
majira ya katikati ya saa nne na saa tano asubuhi wakati Askofu wa
Kanisa hilo akiendelea na ibada. Ibada hiyo sambamba na uzinduzi husika
imeahirishwa hadi wakati mwingine.
Balozi wa Papa na ujumbe wake
walikuwa miongoni mwa wageni muhimu katika tukio hilo la uzinduzi.
Balozi huyo (tutakupatia jina lake baadae) alikuwa Arusha tangia
alahamisi ya Mei 2, 2013 na alipatiwa ulinzi wa kutosha na Jeshi la
Polisi.
Haijaweza kuthibitika hasa sababu za wahusika kurusha “bomu” lakini mmoja wa washukiwa tayari ametiwa nguvuni na Polisi.
Taarifa
kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa takribani watu wawili wanahisiwa
kuwa wamefariki na makumi wengine kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa
hopsitali ya Mt Meru kwa matibabu.
Viongozi mbalimbali wa kijamii
na kiserikali wameweza kufika eneo la tukio, miongoni mwao akiwemo Mkuu
wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, Meya wa Manispaa ya Arusha, Gaudence
Lyimo, na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Gobless Lema.
Wengine ni
Mbunge wa Arumeru Mashariki, mh Joshua Nassari, Diwani Msofe wa Kata ya
daraja Mbili (CHADEMA), diwani wa Kata ya Olasiti na viongozi wengine wa
Jeshi la Polisi na usalama Mkoa na Wilaya.
Jengo la kanisa halijadhurika lakini taharuki miongoni mwa watumiaji wa jengo hilo wakiwemo waumini wa kaisa hilo ni kubwa.
Chanzo
cha mlipuko huo inasemekana kuwa kuna gari ndogo ilifika
kanisani hapo na kusimama. Baadae alishuka mtu aliyekuwa
amevalia vazi mithili ya kanzu na kurusha kitu kuelekea
kanisani ambacho ndicho kilichosababisha mlipuko huo..
Lema hospitaliniMbunge
wa Arusha mjini Godbless Lema akiwa na mbunge wa Arumeru Joshua Nassari
wametoa damu kwa ajili ya majeruhi walioumia katika mlipuko huo.
Lema
amewahimiza wakazi wa Arusha na vijana kujitolea kwa wingi kuchangia
damu ili kuokoa maisha ya majeruhi. Watu wengi wameitikia wito na
wanaendelea kujitolea kuchangia damu kama ishara ya kumuunga mkono
mbunge wao. |
No comments:
Post a Comment