Tuesday, May 14, 2013

WADAU WA TWITTER MPO?, MENGI KUTOA MILIONI MOJA KILA MWEZI

Upo kwenye Twitter? Kama haupo fanya haraka ujiunge sababu kuna ulaji huko!! Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi amesema kuanzia mwezi huu, atakuwa akitoa shilingi milioni 1 kwa kila tweet itakayomfurasha.
Mengi anataka umkune mtima wake kwa tweet yenye akili ambayo inaweza kuchangia kwa namna moja ama nyingine kupunguza umaskini uliokithiri nchini.
“Umaskini umekuwa sugu. Kwa mwaka1 kuanzia Mei nitatoa sh1m kila mwezi kwa tweet nitakayochagua kuwa bora kushinda vita dhidi ya umaskini,” ametweet leo.
Ameongeza kuwa Tweet hiyo iende kwake, yaani mtu akiandika tweet afanye kummention ili aione. Hiyo ndiyo habari ya mjini....kazi  kwenu wazee wa Twiraaaaa..........

No comments:

Post a Comment