Wednesday, May 15, 2013

ZITTO KABWE APIGA MARUFUKU WABUNGE WA CHADEMA KUISIFIA SERIKALI YA CCM!

Tumekuwa na uungwana wa kitambua juhudi mbali mbali za serikali katika kuleta maendeleo nchini. Mara kadhaa Mimi binafsi, Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Wabunge wa CHADEMA tumekuwa tukitambua juhudi hizo. Hata hivyo "appreciation" yetu ya nia njema Kabisa imekuwa ikichukuliwa kisiasa na Mawaziri wa CCM na hivyo kutubeza. Leo Waziri Magufuli kaja na flash disk yenye kauli ya ndugu Mbowe huko Hai. Pia kabeza wabunge wengi wa upinzani. Nikiwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni, nimeagiza kwamba kuanzia Leo Ni marufuku Kwa mbunge wa CHADEMA ku appreciate kazi ya Serikali. Uungwana wetu usitumike kutuponza. Tufanye kazi yetu ya kuisimamia Serikali

No comments:

Post a Comment